[Intro]
Woo!
Uh
A.K.A. Mimi
Ngwair
Na East Zoo
Mzee wa ma-doo (What?)
Bongo Records
[Chorus]
Mademu wangu wote mimi nawazimia
Nipeni namba zenu wote nitawapigia
Sijali kabila bali zenu tabia
Na uzuri wenu ndio vinavyo nivutia
Mademu wangu wote mimi nawazimia
Nipeni namba zenu wote nitawapigia
Sijali kabila bali zenu tabia
Na uzuri wenu ndio vinavyo nivutia
[Verse 1]
Na mademu wengi wa kila aina
Hadi mmoja wa kichina, Na-
Achana na kina Tina, Nina, Phina (?) Dina
Wapo wengi hadi wengine nimewasahau hata majina (Woo!)
Kuna Sabrina 'demu wangu wa Kikurya
Tatizo ana hasira sana
Na kila siku kudundana, kupigana, ndivyo mapenzi yetu yanavyo kwenda
Na sio ka demu wa Ki-Chagga (What?)
Ameenda shule (Yeah)
Bomba, halafu mjanja 'ila anachonikera
Hatuwezi kuelewana siku nsipokuwa na hela
Sio Sintah, ni Anita 'demu wangu wa Ki-Nyaturu, mkorofi ka kijita
Na Mfipa, mbali ya uzuri wake na mapenzi anayonipa (Uh-Huh)
Napenda jinsi anavyo jua kupika
Demu wangu wa ki-Tanga, nampenda anajua sana mapenzi (Yo!)
Urefu ndio kigezo kwa dеmu wangu wa Ki-Nyamwezi
Wapo wengi na 'kwa hali na mali wote, Ngwair nawaеnzi tu
Kwani wote nawapenda sana, kama' nnavyozipenda Makumbusho na K'Nyama
[Chorus]
Mademu wangu wote mimi nawazimia
Nipeni namba zenu wote nitawapigia
Sijali kabila bali zenu tabia
Na uzuri wenu ndio vinavyo nivutia
Mademu wangu wote mimi nawazimia
Nipeni namba zenu wote nitawapigia
Sijali kabila bali zenu tabia
Na uzuri wenu ndio vinavyo nivutia
[Verse 2]
Na mademu wengi hadi nadata
Hata sijui (ni?) vipi mapenzi
Na 'wote wananitaka (Wote wananitaka)
Sijui yupi niwe nae, yupi nimtose (What?)
Kwani hakuna ambae amekamilika sifa zote (Uh-Huh)
Mfano mfupi wa demu wangu wa Ki-luguru, ndio chanzo cha kumwaga na kumchukua wa Ki-mbulu
Na 'nashukuru kupata demu wa Ki-ngoni, msomi na sio kama demu wangu wa Ki-gogo (Yeah)
Kuomba yeye ndio fani, anaweza pika ugali bomba halafu mboga mpaka akaombe kwa jirani (Woo!)
Na Mmanyema kwa kuchonga soo
Na kuna wengi ambao sijajua tabia zao, bro
Ingawa huwa nazingatia tabia (Uh-Huh)
Napenda pia awe mzuri wa kuvutia (Say what?)
Ikiwezekana awe mzuri kupindukia
Yaani hata nikiwa [&@#*], niwe najisikia raha
Na mpaka leo stori hii nawapatia na mademu kama tisa hivi bado nawafukuzia, yeah
Ha-ha-ha, Ha-ha, aah
East Zoo y'all
[Chorus]
Mademu wangu wote mimi nawazimia
Nipeni namba zenu wote nitawapigia
Sijali kabila bali zenu tabia
Na uzuri wenu ndio vinavyo nivutia
Mademu wangu wote mimi nawazimia
Nipeni namba zenu wote nitawapigia
Sijali kabila bali zenu tabia
Na uzuri wenu ndio vinavyo nivutia
[Verse 3]
Wengine niliwapata wakati bado niko Dom
Wengine kwenye shoo nilipo kwenda ku-perform
Wachache wanajulikana mpaka home
Lakini hakuna ambae sikutumia Condom
Na mademu wengi kila sehemu (Kila sehemu)
Hata simu yangu yenyewe imejaa namba za mademu tu (Uh)
Napenda figure ya demu wangu wa Ki-Haya
Wala sijali mnavyo muita yeye malaya
Na Mpare, 'mbishi sana
Demu wangu wa Ki-Rangi nae ana wivu sana
Asione nimesimama na msichana
Hatakama tunaongea dili za maana, 'ishakuwa lawama
Na Msandawe, 'mcheshi sana
Ila lugha ndio kitu tunacho shindwa kuelewana
Kama [****], yaani huwa sijui ana maana gani
Labda ni "I love you, honey" (Haha)
Na Mzaramo kila wiki, ngomani
Bora demu wangu wa Ki-Pemba, yeye kutwa yupo ndani (Yeah)
Msi-mind sana kwa wale niliowasagia
Ila muamini kwamba wote nawazimia
[Chorus]
Mademu wangu wote mimi nawazimia
Nipeni namba zenu wote nitawapigia
Sijali kabila bali zenu tabia
Na uzuri wenu ndio vinavyo nivutia
Mademu wangu wote mimi nawazimia
Nipeni namba zenu wote nitawapigia
Sijali kabila bali zenu tabia
Na uzuri wenu ndio vinavyo nivutia
[Outro]
Haha, yo
Ngwair
Na hii ni kwa ma-player
Nia yangu mi nikutaja makabila tu
So take care, uh-huh
Ha, yeah, baadae
Yo, peace kwa ma-doo na machizi wa East Zoo
Daudi Mavure pamoja na K.U.U